PENATI ya Dakika ya 5 imewapa Liverpool ushindi wa Bao 1-0 walipocheza na Augsburg ya Germany Uwanjani Anfield katika Mechi ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya UEFA EUROPA LIGI na kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16.
Kwenye Mechi ya kwanza iliyochezwa huko Germany Wiki iliyopita Timu hizi zilitoka Sare 0-0.
Penati hiyo ya Liverpool ilifungwa na James Milner na ilitolewa kwa madai kuwa Mchezaji wa Augsburg aliunawa Mpira.
Liverpool watamjua mpinzani wao kwenye Raundi inayofuata baada ya Droo itakayofanyika leo ijumaa Februari 26 huko Nyon, Uswisi.

No comments:
Post a Comment