Wednesday, 2 March 2016

MATOKEO YA MECHI ZA LIGI KUU UINGEREZA

VINARA wa Ligi Kuu England Leicester City Jana wakiwa kwao King Power Stadium walitoka Sare 2-2 na West Brom wakati Ugenini Mabingwa Watetezi Chelsea wakiibwaga Norwich City.
WBA walitangulia kuifunga Leicester kwa Bao la Dakika ya 11 la Salomon Rondon na Leicester kujibu kwa Bao 2 za Danny Drinkwater na Andy King katika Dakika za 30 na 46 na kuongoza 2-1 hadi Haftaimu.
Craig Gardner alifunga Bao kwa Frikiki na kuipa WBA Sare ya 2-2 ambayo imewaacha Leicester wakiongoza Ligi Pointi 3 mbele ya Tottenham ambao Leo wanaweza kutwaa uongozi ikiwa wataifunga Ugenini Upton Park West Ham.


Jumatano Machi 2
2245 Arsenal v Swansea                 
2245 Stoke v Newcastle                  
2245 West Ham v Tottenham         
2300 Liverpool v Man City               
2300 Man United v Watford
Jumamosi Machi 5
1545 Tottenham v Arsenal

No comments:

Post a Comment