Wednesday, 9 March 2016

ARSENAL YATINGA ROBO FAINAL FA CUP

MABINGWA Watetezi wa Emirates FA CUP Arsenal Jana waliichapa Hull City 4-0 huko KC Stadium katika Mechi ya Marudiano ya Raundi ya 5 na kutinga Robo Fainali.

Timu hizo zilitoka 0-0 huko Emirates na kulazimika kurudiana.

Bao za Arsenal hapo Jana zilifungwa na Olivier Giroud na Theo Walcott, kila mmoja akipiga 2.
Kwenye Robo Fainali Arsenal wapo Nyumbani kucheza na Watford.


No comments:

Post a Comment